Hatahivyo kiongozi wa mapinduzi hayo jenerali Godefroid Niyombare ametoroka na anasakwa kulingana na msemaji wa rais.
Awali Jenerali Niyombare alikiambia chombo cha habari cha AFP kwamba yeye na wafuasi wake watajisalimisha akiongezea kuwa ''natumai hawatatuua''. Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema kuwa amerudi nchini BurundI na kwamba anatarajiwa kulihutubia taifa.
Swali kubwa ni JE? Uchaguzi utafanikiwa kama ulivyopangwa?
Tazama 'Tweet' yake aliyoituma kupitia mtandao wa Twitter kuthibitisha kurudi kwake nchini Burundi.
kdhjg