Tetemeko la ardhi Nepal laongeza masaibu

May 13, 2015

 
Serikali ya Nepal imetoa wito wa kuwepo hali ya utulivu nchini humo baada ya tetemeko kubwa la ardhi kuikumba tena nchi hiyo na nchi jirani hapo jana. Maafisa wa jeshi la majini la Marekani wamesema helikopta ya Marekani ya kutoa misaada iliyokuwa na abiria wanane haijulikani iliko baada ya tetetemeko hilo jipya. Tetemeko hilo la kiwango cha 7.3 katika kipimo cha Ritcher limeongeza masaibu ya raia wa Nepal wiki chache tu baada ya jingine kuwaua maelfu ya watu. Maafisa wa Nepal wamesema kiasi ya watu 48 wameuawa hapo jana na kiasi ya wengine 1,176 wamejeruhiwa huku majengo kadhaa yakiporomoka. Wafanyakazi wa shughuli za uokozi wametumwa katika maeneo yaliyoathirika na mkasa. India na China pia zimeripoti kuathirika na tetemeko hilo la ardhi. 

Idhaa ya DW
Share on :
 
Copyright © 2015 Raizoni Blog
Distributed By My Blogger Themes | Design By SPARTO Inc Team