
Akijibu
swali la Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Susan Lyimo, mtendaji mkuu wa Serikali Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda
alitetea ushiriki wa watoto wapatao 500 kwenye sherehe hizo akisema ni sehemu
ya mfumo wa wanachama wa CCM.
“Susan,
utafikiri tulikuwa pamoja. Nilijua tu swali hili lazima litaulizwa. Ila ‘mtoto
wa nyoka ni nyoka’. Chama hiki kina mfumo wake ambao umeshuka mpaka kwenye
ngazi ya kitu kinaitwa chipukizi,” alisema akijibu swali la mbunge huyo
aliyetaka kujua sababu za CCM kutumia watoto kwenye shughuli zake za siasa
wakati ina wanachama wapatao milioni 10 kote nchini.
“Chipukizi
hawa ni watoto ambao wamezaliwa kutokana na wazazi wana-CCM, ndiyo maana chama
kiliwatumia. Sherehe ilikuwa nzuri na ilipendeza sana. Kwa kuwa hawajafikia
umri wa kuingia katika masuala ya siasa, halina madhara lile rafiki yangu, pia
bado ni wadogo mno na walikuwa wanafurahia gwaride na kuvaa sare tu.”
Lyimo
hakuridhishwa na jibu hilo la Waziri Pinda, akisema hakutakiwa kutoa majibu ya
aina hiyo na kwamba katika mkusanyiko huo, kulikuwa na watoto ambao wazazi wao
siyo wanachama wa CCM.
“Lengo
la watoto hawa ni kusoma na siyo kufanya siasa. Iweje mfanye mambo kwa double
standard (ndumilakuwili)?” alihoji na baadaye Pinda alitaka suala hilo
lisiendelee kujadiliwa.
“Naheshimu
maelezo ya Susan, lakini kiacheni chama kiendelee na utaratibu wake. Mfumo wake
ndiyo huo, ndivyo ulivyo na sidhani kama kuna haja ya kuendelea kubishana
katika suala hili,” alisema Pinda ambaye ofisi yake inasimamia elimu ya msingi
na sekondari.
Najitahidi
kuamini kila mwanafunzi alileta kitambulisho cha uanachama cha mzazi wake kuhakikisha uwiano
wa maelezo ya Waziri Mkuu na uhalisia.
KARIBU MWEZI OKTOBA!