Aliyelipua bomu 2013 ahukumiwa Kifo!

May 16, 2015

screen grab from V Kontakte - fair use

Dzhokhar Tsarnaev kijana wa umri wa miaka 21 aliyetuhumiwa kwa kosa la kulipua bomu wakati wa Mashindano ya Mbio katika mji wa Boston mwaka 2013 amehukumiwa adhabu ya kifo!
Hukumu hiyo iliyosomwa na jaji George O'Toole ilionyesha mshtakiwa alipatikana na makosa 6 yaliyopelekea kupewa adhabu hiyo.
Bado hukumu ya kifo hajasomewa rasmi ingawa kuna habari za kuweza kupelekwa katika mji wa Terre Haute, Indiana ambapo hukumu yake itatekelezwa. Mpaka kufikia mwisho wa kesi hii, wiki zaidi ya 10 zilitumiwa ndani ya mahakama kwa mashahidi 150 kutoka ushahidi wao huku mamia ya vielelezo ikiwemo video na picha vikitumika katika maamuzi.
Bomu lililolipuka Boston lilitengenezwa na 'pressure cooker', misumari na unga wa risasi ambapo ujuzi huu wa utengenezaji ulisomwa kutoka Online Magazine ya kundi la al Qaeda linayoitwa "Build a Bomb in the Kitchen of Your Mom." au ''Jinsi ya kutengeneza Bomu katika Jiko la Mama Yako''. Watu zaidi ya 240 walijeruhiwa na 17 zaidi kupoteza miguu yao.
Angalia Tweets za baadhi ya waathirika wa bomu hilo walizotuma baada ya taarifa ya hukumu kutolewa;

My mother and I think that NOW he will go away and we will be able to move on. Justice. In his own words, "an eye for an eye".

Several of the survivors & family members dab tears from their eyes. Martin & Denise Richard did not want death. They look stoic.
Share on :
 
Copyright © 2015 Raizoni Blog
Distributed By My Blogger Themes | Design By SPARTO Inc Team