Machafuko Burundi: Nkurunzinza atoa amri

May 10, 2015

Waandamana kumpinga Nkurunziza nchini Burundi

Baraza la usalama la kitaifa nchini Burundi limesema watu hao waache uasi wao unaoyatatiza maisha ya watu wa Burundi. Waandamanaji wamepewa muda wa saa 48 kiviondoa vizuizi vyote walivyoviweka barabarani.
Baraza hilo la usalama linaloongozwa na Rais Nkurunziza limetaka njia zote zilizowekewa vizuizi na wapinzani hapo awali zifunguliwe na majeshi ya usalama, katika muda wa saa 48.
Lakini kiongozi wa upinzani Pacifique Nininahazwe ameishutumu amri hiyo iliyotolewa na serikali na ameiita kuwa ni tangazo la vita. Bwana Nininahazwe amesema maandamano yataendelea hadi hapo Rais Nkurunziza atakapouacha mpango wake wa kuwania muhula wa tatu wa urais unaoenda kinyume na katiba ya nchi.
Share on :
 
Copyright © 2015 Raizoni Blog
Distributed By My Blogger Themes | Design By SPARTO Inc Team