Dar es Salaam. Hatimaye Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) imeweka hadharani ratiba nzima ya uandikishaji wapigakura
kwa kutumia teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR) huku mkoa
wa Dar es Salaam ukipangiwa siku 12 tofauti na mwezi mmoja uliotumika
katika mikoa mingine.
NEC imetoa ratiba hiyo baada ya kuwepo mashinikizo
kutoka kwa wadau na ikiwa ni miezi mitatu tangu ilipoanza kuandikisha
kitaifa mkoani Njombe, Februari 23 kwa kuandikisha watu 300,800.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo iliyotolewa jana na Mkuu
wa Idara ya Habari na Elimu kwa Mpiga Kura, Ruth Masham, wakazi wa Dar
es Salaam wataanza kujiandikisha kuanzia Julai, 4 hadi Julai 16 mwaka
huu.
Siku hizo ni pungufu kwa siku 16 kutoka katika
wastani wa siku 28 ambazo zinatumika Lindi na Mtwara au Ruvuma na Iringa
licha ya jiji hili kuwa na watu wanaokadiriwa kuwa na umri wa kupiga
kura zaidi ya 2.93 milioni, kwa mujibu wa Shirika la Taifa la Takwimu
(NBS).
Mwanachi
Mwanachi