Dar es Salaam siku 12 tu kujiandikisha kupiga kura!

May 23, 2015



Dar es Salaam. Hatimaye Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeweka hadharani ratiba nzima ya uandikishaji wapigakura kwa kutumia teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR) huku mkoa wa Dar es Salaam ukipangiwa siku 12  tofauti na mwezi mmoja uliotumika katika mikoa mingine.
NEC imetoa ratiba hiyo baada ya kuwepo mashinikizo kutoka kwa wadau na ikiwa ni miezi mitatu tangu ilipoanza kuandikisha kitaifa mkoani Njombe, Februari 23 kwa kuandikisha watu 300,800.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo iliyotolewa jana na Mkuu wa Idara ya Habari na Elimu kwa Mpiga Kura, Ruth Masham, wakazi wa Dar es Salaam wataanza kujiandikisha kuanzia Julai, 4 hadi Julai 16 mwaka huu.
Siku hizo ni pungufu kwa siku 16 kutoka katika wastani wa siku 28 ambazo zinatumika Lindi na Mtwara au Ruvuma na Iringa licha ya jiji hili kuwa na watu wanaokadiriwa kuwa na umri wa kupiga kura zaidi ya 2.93 milioni, kwa mujibu wa Shirika la Taifa la Takwimu (NBS).

Mwanachi
Share on :
 
Copyright © 2015 Raizoni Blog
Distributed By My Blogger Themes | Design By SPARTO Inc Team